Friday, April 26, 2013

STANLEY MSUNGU AKERWA NA WAUZA SURA KWENYE FILAMU.

Stanley Msungu muigizaji anayefanya vizuri katika tasnia ya filamu amesema kuwa anakerwa na wauza sura katika filamu ambao hawana vipaji na hawako serious katika kuiendeleza tasnia ya filamu ili ikue. Muigizaji huyo aliyeigiza katika filamu nyingi kama vile Ndoa Yangu, Devil Kingdom, Stuck on You na nyinginezo aliyasema hayo alipoulizwa na SWP ni kitu gani hakipendi kwenye tasnia ya filamu kwakuwa hakina tija katika tasnia hiyo. "kuna watu wanaonyesha sura hawafanyi kazi". Tatizo hili limekuwa likilalamikiwa na wadau wengi kiasi cha baadhi ya filamu zenye wauza sura zikikosa mvuto kwa kuwa hakuna ushawishi wa kisanaa kutoka kwa waigizaji husika.


No comments:

Post a Comment