Wednesday, April 24, 2013

BATULI AUMIZWA NA GAZETI LA SANI KWA KUANDIKA KUWA ANA KANSA YA TITI.

Muigizaji Yobnesh Yusuph( Batuli) ameonekana kuumizwa na gazeti la Sani la leo kwa kuandika katika ukurasa wa mbele wa gazeti hilo kuwa ana kansa ya titi na muigizaji huyo kukanusha. Mashabiki wake pia walikuwa wameshaanza kujawa na simanzi wakijua ni kweli lakini muigizaji huyo amekanusha live.  Hata hivyo Swahiliworldplanet hatukuisoma bado habari hiyo ndani ya gazeti hilo zaidi ya kuona kichwa cha habari juu ya gazeti hilo lakini tunalitafuta ili kuisoma habari nzima.


No comments:

Post a Comment