Wednesday, November 5, 2014

Photos: Nisha Ashuti Filamu Mpya Huko Zanzibar.

Star mkubwa wa filamu Tanzania Nisha Salma Jabu hivi juzi kati alikuwa Zanzibar kwa ajili ya kufanya kazi ya filamu na Zanzibar House Of Talent katika kuinua vipaji vipya ukifikiria mwenyewe anatokea visiwani humo. Nisha alisema bado hajaridhika na mafanikio aliyopata kupitia filamu kwani shida yake sio umaarufu bali kuwa mwanamke mwenyewe mafanikio.......


"saa nyingine nafikiria Angelina Jolie huyu hapa, na wakati mwingine nawaza Genevieve Nnaji au Mercy Johnson huyu hapa, ila Inshallah Mwenyezi Mungub atanifungulia kwa kila ndoto niiotayo leo na ndio maana kufanya kazi kwa bidii na kuwa mbunifu na kutokuchoka na kuridhika ndo wamekuwa marafiki zangu wakubwa 'I wanna be a successful woman'" alisema Nisha wakati akichonga na Swahiliworldplanet. Angalia picha wakati akishuti filamu hiyo huko Zanzibar


No comments:

Post a Comment