Saturday, November 8, 2014

Breaking News: Sitti Mtemvu Ajivua Rasmi Taji La Miss Tanzania 2014, Lilian Kamazima Kuchukua Taji Hilo.

Sitti Mtemvu
Hatimae Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu amejivua rasmi taji la Miss Tanzania baada ya kuandamwa na kashfa ya kudanganya umri. Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim Lundenga ametangaza hilo leo hii katika mkutano na waandishi wa habari baada ya kupokea barua toka kwa Sitti mwenyewe kuamua kulivua taji hilo.
Kwa mujibu wa Lundenga mshindi wa pili Liliani Kamazima ndie atachukua taji hilo licha ya Jihan Dimachk kupewa nafasi kubwa ya kutwaa taji hilo wakati wa shindano hilo ambapo aliambulia nafasi ya tatu na watu kudai alionewa.


No comments:

Post a Comment