Friday, October 31, 2014

Wema Sepetu Na Diamond Platnumz Wamwagana ! Sababu Hii Hapa.

Diamond Platnumz na Wema Sepetu wanadaiwa kumwagana kimtindo kwa mujibu wa gossip mpya. wawili hao inasemekana hawapo kwenye mahusiano mazuri na inaelekea wamemwagana
huku chanzo kikidaiwa ni BMW alilopewa Wema kama zawadi toka kwa Martin Kadinda siku ya birthday yake lakini ikidaiwa kutoka kwa mwanaume mwingine. Pia hivi majuzi Wema alienda China lakini licha ya kuongozana na Kadinda na Petitman anadaiwa kuongozana pia na wanaume wawili wanaohisiwa kumuwezasha kipesa zaidi Wema kwani Diamond sio mtu wa kumwaga pesa hovyo bila sababu za msingi kama yule kigogo wa ikulu kwa mujibu wa chanzo.

Madai zaidi yanasema kuwa katika birthday ya Aunty Ezekiel juzi Wema na Diamond kila mmoja alimlia bati mwenzake bila kuchangamkiana kwa salamu wala nini ukumbini na Wema aliingia ukumbini hapo maeneo ya Masaki akitokea Dubai.

Vilevile Wema alidaiwa kumuomba Diamond mtaji lakini bado alikuwa hakupewa kwa wakati.


Like our Facebook page Swahili World Planet for more updates about Tanzanian movie stars' latest gossips, news, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment