Thursday, October 2, 2014

Cathy Rupia Atibuliwa ! Afunguka Mpaka Basi.

Sabrina Cathy Rupia ametibuliwa !....muigizaji huyo mwenye kipaji na mkongwe kupitia Instagram ameandika maneno hayo hapo chini dhidi ya mtu flani mwenye chuki binafsi nae kutaka abaniwe kupata deals za filamu........

"Wenye chuki binafsi na mimi kutaka kujaribu kunibania kwenye kazi hasa wewe kaka fulani jua kwangu umechemka ninavyohangaika kwa kazi za mikono yangu jua kama Mungu kapanga Yes itakua Yes tuu nina maeneo mengi yakupatia ugali mpare nahangaika we unatia fitina utachomwa na Moto wa jahanam ukiwa bado unatembea unamchekea mtu mdomoni wakati moyoni unamuombea mabaya nenda tuone kama ukirudi utabadilika nini ! Kujifanya swala 5 kumbe loo beduli kama yeye hakuna mnafiki ni mbaya kuliko mchawi wewe ni nyoka unaua na huli kila siku kama unavuta mi nabwia jipange kaka na nisikie ukinitaja jina langu huko utanijua vizuri angalia wakumchezea, eti oohh pale Cathy hafiti jamani alafu ukiwa namie unajichekesha dada dada kumbe unanilamba kidogo kwendaaaaa."


Like our Facebook page Swahili World Planet for more updates about Tanzanian movie stars' latest gossips, news, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment