Thursday, November 21, 2013

LUPITA NYONG'O KAMA ANGEKUWA TANZANIA ASINGEWEZA KUPEWA NAFASI KATIKA FILAMU ZA KIBONGO.

Lupita
Kipaji cha kweli siku zote huonekana hata kama itachukua muda mrefu. Lupita Nyong'o kutoka Kenya ameiteka Hollywood ndani ya muda mfupi tu kutokana na performance yake hatari katika filamu ya 12 Years A Slave. Lupita mwenye weusi hasa wa kiafrika au ule wa kisudani kila media nchini marekani na nje zinataka kufanya nae interviews kuanzia majarida ya filamu, mitindo na vipindi vya Tv vyote vinaonekana kutekwa na msanii huyu chipukizi kutoka Africa mashariki. Filim critics wanampongeza kwa performance yake kwenye hii filamu kiasi cha kutabiriwa nominations za tuzo zote kubwa zikwemo Oscars katika kipengele cha Best supporting actress, fashion critics nao hawapo nyuma kumpa kudos huku majarida yote makubwa ya mitindo yakipigana vikumbo kufanya nae photoshoot na interviews.

Hata kabla filamu ya 12 Years A Slave kutoka nilivutiwa sana na trailer yake kwa kumuona Lupita labda kwa kuwa napenda sana filamu za kihistoria zikiwemo za kuzungumzia Slave Trade na baada ya filamu hiyo kutoka Lupita akawa an overnight star in Hollywood. Am sure Lupita kama angekuwa hapa Tanzania(Bongo) asingepewa nafasi na watengeneza filamu wa hapa kutokana na muonekao wake wenye asili ya kiafrika hasa na umbo dogo la wastani, kwanza angeambiwa labda ajichubue awe mweupe, anenepe awe na makalio ya kichina au umbo lake ni dogo hawezi kucheza nafasi za mke wa mtu kama tulivyoshudia Mainda akiambiwa umbo lake ni dogo ndiyo maana hapewi nafasi muhimu. Tunao kina Lupita wengi tu hapa nchini lakini hawapewi nafasi eti hawauzi au wana sura mbaya na hao wanaoitwa mastaa wa filamu vipaji hawana ila wapo kwa ajili ya kukuza majina yao kwa skendoz na kuuza makava ya filamu.
Mfano Jenifer yule mtoto aliyekuwa akiigiza na Kanumba na kuonyesha kipaji cha hali ya juu na kuvuta mashabiki wengi mpaka nje ya nchi tayari amepotea baada ya Kanumba kufariki lakini mtoto yule ana uwezo wa kufanya maajabu hata Hollywood.

Lupita Leo hii tayari ni star mkubwa wa filamu kupitia filamu moja tu tena akiwa amecheza kama mhusika msaidizi, amewamwaga mastaa wengi wa Tanzania, Nigeria na Ghana kwa ustaa huko mtoni. Ukiachilia mbali kipaji na muonekano wake wa asili kingine kilichomsaidia Lupita ni kuwa na elimu nzuri katika tasnia ya filamu kwani amesomea mambo ya filamu. I THINK muda umefika sasa kwa watengeneza filamu Tanzania kuangalia kipaji cha kweli na sio uzuri wa sura na umbo kupewa kipaumbele kuliko kipaji ili hata msanii akianza katika filamu zetu basi iwe rahisi kuwika kimataifa akipata nafasi hiyo huku waigizaji wenyewe wakitakiwa kuongeza elimu na bidii ya kazi. Hii ni kwasababu kuna wanaoitwa mastaa wakubwa wa filamu Tanzania lakini hawana vigezo vya kuwika kimataifa wala vipaji vyao havionekani licha ya kucheza filamu kibao, yaani umaarufu wao ni mkubwa kuliko uwezo wao wa kuigiza.
Lupita akiwa katika filamu ya 12 Year A Slave........
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment