Sunday, May 18, 2014

Anayoyafanya Nisha Mastaa Wenzake Wengi Huwashinda !

Muigizaji wa filamu mwenye jina kubwa nchini Salma Jabu Nisha hajulikani tu kwa kazi zake za filamu bali anajulikana pia kwa kujitoa katika matukio mbalimbali ya kijamii ikiwemo kusaidia wasiojiweza na watoto yatima mara kwa mara kitu ambacho hufanywa na wasanii wachache sana. Jana katika msiba wa msanii mwenzake Adam Kuambiana, muigizaji huyo aliweka u-star wake pembeni na kujitosa kupika maandazi kama anavyoonekana pichani.

Nisha akiwa na mke wa marehemu Adam Kuambiana
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Kwa upande mwingine filamu mpya ya Nisha inayoitwa ZENA NA BETINA imepengwa kutoka tarehe 29 mwezi huu.

No comments:

Post a Comment