Wednesday, January 29, 2014

SHILOLE APATA MPENZI WA KIZUNGU, ASEMA NILIPOKUWA NAPATAKA NIMEFIKA.

Shilole ambaye ni star wa filamu na muziki nchini Tanzania amenasa kwenye penzi la jamaa wa kizungu raia wa Uingereza anayejulikana kwa jina la Ankar. Jamaa huyo kwa mara ya kwanza alidatishwa na shilole katika show aliyoifanya nchini Uingereza. Chanzo kimoja kikizungumza na Globalpublishers kilisema "Ukweli ni kwamba Shilole ana mchumba wa Kizungu na walikutana kwenye shoo ya mara ya kwanza aliyoenda kufanya nchini Uingereza na hivi karibuni ataenda tena na amealikwa na huyo mchumba wake"

Naye Shilole alipoulizwa na mtandao huo alisema " Kweli nina mchumba Mzungu ambaye ni raia wa Uingereza, nilipokuwa napataka nimefika, sipindui tena. Unajua muziki wangu na mauno yangu yanawavutia sana watu, siku ya kwanza aliniona kwenye shoo akanipenda ndipo tukaanzisha urafiki, Hivi karibuni nina safari ya kwenda nchini humo kwa mwaliko maalum alionipa, nitaenda peke yangu kwani safari nyingine zote zilizopita nilikuwa naenda na watu,” alisema Shilole"

                             Shilole na mpenzi wake huyo

Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment