Friday, February 28, 2014

Navutiwa Zaidi Na Wanaume Weusi na Sio Weupe: Wema Sepetu

Wema Sepetu
Wema Sepetu amesema kuwa yeye mzuka wake upo kwa wanaume weusi zaidi na sio wanaume weupe. Akizungumza kwenye kipindi cha Leo Tena kinachorushwa na radio Clouds Fm Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 ambaye pia ni star wa filamu Swahiliwood aliulizwa mwanaume mwenye sifa gani anayevutiwa nae na kuweza kumuoa, Wema alijibu "Kuolewa sio shida je huyo mwanaume nampenda,maana naweza kuja kuchumbiwa lakini nisimpende, Mimi nampenda Mwanaume mweusi,wanaume weupe sio kwamba sijawahi kuwa nao lakini nakuwa sina mzuka nao"


Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake wa kimapenzi na Diamond Platinumz mrembo huyo asiyekauka kwenye media alisema " Kweli niko na Nasib - Diamond na nadhani muda huu kutakua na utulivu ndani yake,ule utoto tuliokua tunafanya nadhani ulikuwa utoto na imekua Power Couple toka mwaka 2010 kwa hiyo tuna ni miaka 4 sasa,kwa sasa tumeamua kuwa serious"

Wema na Diamond
 
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment