Friday, November 7, 2014

Ukaribu Wangu Na Kajala Haimaanishi Nina Beef Na Wema Sepetu: Jackline Wolper

Wolper
Star mwenye mvuto wa hali ya juu kunako tasnia ya filamu Tanzania, Jackline Wolper amesema kuwa hana beef na Wema Sepetu kama inavyovumishwa na watu kwakuwa tu yupo karibu na Kajala ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Wema Septu kabla ya kuingia katika beef zito.

Akizungumza na Globalpublishers Wolper ambaye kwasasa anatesa sokoni na filamu yake mpya ya V.I.P alisema
"Ujue watu wengi sana wamekuwa wakidhani mimi na Wema tuna bifu, sijui kwa kuwa mimi nina ukaribu na Kajala au kwa kuwa hatujawahi kuwa pamoja, lakini ukweli mimi na Wema siyo waongeaji sana japokuwa huwa nikiweka picha au chochote kwenye Instagram, Wema huwa ana-like na mimi huwa na-like vitu vyake hivyo sidhani kama nilikuwa na tatizo naye sana"

No comments:

Post a Comment