Wednesday, November 5, 2014

Hii Ndio Sababu Inayodhihirisha Kuwa Shilole Na Nuh Mziwanda Hawawezi Kuoana Bali Wanachezeana Tu !

Shilole na Nuh Mziwanda
Tofauti ya dini inaonekana kuwa kikwazo kwa ndoa ya Shilole na Nuh Mziwanda , wawili hao walipozungumza na GPL walikuwa na mitazamo hii

"Mimi ninampenda Shilole kwa asilimia 100,  ila siko tayari kubadili dini kwa ajili yake maana kwetu ni wakristo na hapa naongea mama yangu ni mzee wa kanisa hivyo Shilole naamini anaweza kubadili maana mimi tayari nimeshafanya mengi sana juu yake." alisema Nuh ambaye ni msanii wa Bongofleva

NaeShilole alisema "Mimi siwezi kubadili dini maana Nuh ndiye alisema atabadili hata hivyo familia yangu haiwezi kunikubalia kubadili dini kwa ajili ya kufunga ndoa kama amesema naye hawezi kubadili basi tutaishi tu maana hata ndoa ya serikali yenyewe hawezi na maisha siyo lazima tuoane"

No comments:

Post a Comment