Sunday, September 28, 2014

Mume Wangu Hajanikataza Kuigiza Filamu: Jacque Pentzel.

Jacque na mumewe Gadner Dibibi
Star wa filamu Tanzania Jacquline Pentzel Dibibi akiongea na SWP amesema kuwa mume wake Gadner Dibibi(30) hajamkataza kufanya kazi zake za movies, bali alikuwa kimya kutokana na kusoma game lilivyo sasa. Jacque amesema kuwa hivi sasa yupo kambini maeneo ya mbezi, Dar es salaam akishuti movie yake mpya lakini hakuweka bayana jina la hiyo movie.
Msanii huyo ambaye mashabiki wake wamemzoea kwa jina la Jack Wa Chuzi alibadili dini na kuwa muislam na kufunga ndoa mwanzoni mwa mwaka jana na kijana Gadner Hatwaby Dibibi na kuchagua jina la Kauthar Dibibi ambalo ndio jina lake la ndoa.

                                                                  Jacque

No comments:

Post a Comment