Wednesday, May 7, 2014

Modest Bafite Kuanza Kufanya Filamu Zake Mwenyewe Baada Ya Kukubalika Kwa Mashabiki.

Muigizaji wa filamu nchini Tanzania mwenye asili ya Congo Modest Bafite ambaye pia tayari alishacheza filamu pamoja na marehemu Steven Kanumba anatarajia kuanza kufanya filamu zake mwenyewe baada ya kupata uzoefu na kukubalika vizuri kwa mashabiki. Kupitia mtandao mmoja wa kijamii Modest ameandika. 
"Nashkuru Mungu na wote mlioniunga mkono mpaka hapa nilipo kisanaa, Sasa ni wakati wangu wakufanya kile kilichonitoa Congo kuja Tanzania, muda wowote kuanzia sasa naweza kuanza kufanya filamu zangu Afrika nzima, kuanzia Congo, Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya na Tanzania, Sijaja kuuza Sura kwenye tasnia ya filamu Tanzania, nashukuru maana Filamu nilizocheza zinanipa Umaarufu mkubwa ndo sababu ya kukamilisha ndoto zangu, Kwa ushauri na mengineo, Wasiliana na mimi Modest Bafite bila tatizo, ikiwa hujawahi kuona filamu zangu niulize nitakwambia title ya Filamu ambazo nimecheza, mnakaribishwa kwa maoni"

Kwa upande mwingine filamu mpya ya Modest inayoitwa SIO SAWA itaingia sokoni muda wowote kuanzia sasa ambapo amecheza na mastaa wenzake kama vile King Majuto, Babylove Kalalaa na Salehe Lufedha ambaye ndiye producer wa filamu hiyo kali.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Filamu kali ya SIO SAWA inaingia sokoni Ijumaa hii April 2014 hakikisha unanunua nakala yako halisi.
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and 

No comments:

Post a Comment