Pages

Wednesday, March 19, 2014

Ni Matumizi Mabovu Ya Akili Kwa Msanii Kuwa Busy Na Skendo Badala Ya Kazi: Gabo Zigamba.

Swahiliworldplanet ilipata nafasi ya kuzungumza machache na star wa filamu nchini Salim Ahmed "Gabo Zigamba" kuhusiana na kazi zake za filamu na maisha binafsi hivi juzi kati. Gabo ambaye kipaji chake cha kuigiza hakijifichi huku akiwa tayari amejizolea mashabiki wengi alitiririka kama ifuatavyo katika interview hii ndogo.

SWP: Nani alikushawishi kuingia kwenye sanaa ya uigizaji?

GABO: Ni msukumo wa maisha baada ya plan A na mtazamo wa ndugu jamaa na marafiki

SWP: Umefaidika na nini mpaka sasa tangu uanze kuigiza filamu?

GABO:  Kwa upande wa mafanikio bado naidai sanaa

SWP:  Kitu gani huwa kinakukera zaidi unapokuwa location?

GABO: Kero kubwa ni mijadala ya pre-production ndani production....

SWP: Baadhi ya waigizaji nchini wapo busy kutengeneza skendo ili kuandikwa kwenye media huku kazi zao zikiwa chache na bado haziridhishi je unalizungumziaje hilo?

GABO:  .Ni matumizi mabovu ya akili huwezi kuwa busy na skendo ikiwa huna kaz miliki.....

SWP:  .Umeoa au una mchumba?

GABO:  Nina mke na mtoto mmoja

SWP:  Nini matarajio yako ndani ya miaka 3 ijayo kuanzia sasa?

GABO: Kufanya sanaa kimataifa

  Kwa upande mwingine filamu mpya ya JICHO LANGU aliyoigiza Gabo, Odama na Thadeo Alexernder itaingia sokoni tarehe 31 mwezi huu wa tatu hakikisha unanunua nakala yako hali ya filamu hii mpya kali.

Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment