Saturday, March 15, 2014

Abdallah Mlowezi Zao Jipya Katika Tasnia Ya Filamu Nchini Kutoka Kwa Lucy Komba.

Mlowezi
Baada ya kuwatoa mastaa kadhaa wanaofanya vizuri kwasasa kwenye tasnia ya filamu nchini kama vile Jackline Wolper, Irene Uwoya, Mzee Chilo na wengineo, Lucy Komba tayari ameibua kipaji kingine kipya. Abdallah Mlowezi anayeonekana pichani ndiye msanii mpya aliyeibuliwa na Lucy Komba na tayari ameshaanza kucheza filamu kadhaa na Lucy na mastaa wengine kama Issa Musa "Cloud" katika filamu ya Sim Card na Rose Ndauka katika Rent House. Muigizaji huyo pia amecheza kama daktari katika filamu ya Tanzania To Denmark. Abdallah hupenda kutambulika kama Mlowezi katika tasnia ya filamu.


Mlowezi akiwa location na Cloud katika filamu ambayo alicheza kama muuza chipsi.
 Abdallah akiwa na Lucy Komba
Mlowezi akiwa na Wastara
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment