Wednesday, November 27, 2013

WEMA SEPETU AJUTA KUTUMIA MKOROGO, ATAMANI NGOZI YAKE YA AWALI.

Habari ni kuwa Wema Sepetu ambaye ni Miss Tanzania 2006 na muigizaji wa filamu anajuta kutumia mkorogo na hatimaye kupoteza urembo wake wa asili aliokuwa nao mwanzo kabla ya kuanza kujichubua. Chanzo kimoja makini ambacho kipo karibu na Wema na ambacho pia ni star wa filamu kimeitonya Swahiliworldplanet jana kuwa Wema anajuta kujichubua na hajiamini tena katika urembo tofauti na miaka ya nyuma kwani kila mtu sasa hivi anajua Wema ni fake na amejaa urembo wa kichina kwa aslimia kubwa.

 " Wema mliyekuwa mwamjua kwa kujiamini si huyu wa sasa yaani anajuta kutumia mkorogo baada ya kujeruhiwa na madawa hayo yenye sumu, na zile habari kuwa alienda China kuwekwa ngozi ya bandia zilipoenea ndiyo kabisa zikamvunja nguvu, kiufupi Wema anatamani ngozi yake ya mwanzo sababu wengi wanajua urembo wake ni fake, unajua yule amezungukwa na wanafiki wengi wanamsifia hata katika mambo yasiyo na msingi ndiyo sababu akawa anazidisha mkorogo wakati anasifiwa eti mzuri na ana mvuto, sasa yamemtokea na puani... mimi akhaa! siwezi kuingia kwenye mkumbo huo" kilisema chanzo hicho.


                                                     Wema Sepetu

Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment