Sunday, September 22, 2013

RAYUU KUWEKA HADHARANI UCHAFU WA SINTAH KAMA ATAENDELEA KUMFUATAFUATA.

Rayuu
Kwa wale waliofikiri kuwa beef la waigizaji wa filamu nchini Christina Manongi(Sintah) na Rayuu limekwisha basi wamekosea. Juzi Sintah ambaye pia ni blogger maarufu aliweka picha za nusu uchi za mwamke mmoja anayeitwa Florah Lymo amabye pia ni blogger aliyewahi kudai kubakwa na mbunge mmoja wa kanda ya kaskazini na katika post ya picha hizo Sintah alilitaja jina la Rayuu kwa kuandika "LORD HAVE MERCY , hapana aiseeee mtu mzima kama wewe kweli ukafanye mambo yakina Rayuu?? ni umaarufu wa aina gani unaoutafuta jamani"

 Baada ya kuandika hivyo inaonyesha Rayuu ambaye pia alianzia kuigiza katika kundi la Kaole Kama Sintah alitonywa na watu wake na kuona alichokiandika Sintah hivyo kupitia Facebook Rayuu ameandika "Sintah bila kunitaja hujisikii raha, sitaki uniongelee naona mirembe inakuita, we sio mzima na ukiendelea natoa uchafu wako hadharani"

                                                                   Sintah
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news

No comments:

Post a Comment