Saturday, July 20, 2013

MUIGIZAJI MR.BOMBA AFARIKI DUNIA

Msanii wa zamani wa Kundi la Kaole Sanaa na muigizaji wa filamu Mr.Bomba amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na kansa ya uvimbe wa kwenye ini. 


Msiba utakuwa Buguruni Malapa jijini Dar es salaam nyumbani kwa marehemu alipokuwa akiishi. Mwili utaagwa siku ya Jumatatu nyumbani kwake Buguruni na kusafirishwa kijijini kwao Mpwapwa Dodoma siku hiyo ya Jumatatu kwa mazishi.

                                                         R.I.P Mr.Bomba

No comments:

Post a Comment