Friday, May 3, 2013

LULU ALIJIA JUU GAZETI LA UDAKU LILILOMUANDIKA VIBAYA.

Actress Elizabeth Michael(Lulu) ameonekana kuchukizwa na kitendo cha gazeti moja kumuandika kwa habari aliyoona siyo ya kweli. Gazeti hilo la udaku liliandika kichwa cha habari kisemacho "Lulu, Wema, Diamond afya mgogoro". Katika kujibu na kuelezea hisia zake actress huyo aliamua kuwa mkali kidogo na kusema kuwa Lulu wa sasa sio yule wa Zamani maana amekuwa. ".Imekuwa ni kawaida ya mtu kujisikia kusema chochote...muda mwingine mnaweza mkahisi hatuoni au mkahisi kukaa kwetu kimya ni wajinga!!mm kama mm napenda kuwajulisha kuwa LULU mliyekuwa mnamjua sio LULU wa ss...msitegemee kusikia nabisha au kupigizana kelele...fanyeni kazi yenu lakini sio kuchafuana na kuipotosha jamii....!!!nadhani kimya changu kina majibu mengi" alifunguka Lulu.


No comments:

Post a Comment