Wednesday, July 9, 2014

Sabby Angel Achoka Kutongozwa Hovyo, Kuwachukulia Hatua Wanaomlazimisha Penzi Kwa Nguvu.

Sabby Angel sasa amechoka kutongozwa hovyo ! tena kwa nguvu na baadhi ya wanaume walio kwenye music na movie industry wakimtaka kimapenzi kwa nguvu.


 Habari mpya zinasema kuwa Sabby amechoshwa na tabia hiyo na kama wanaume hao hawatabadilika itafikia hatua atawaanika kwasababu anahisi kama ananyanyasika akiwa kama mwanamke. Inadaiwa kuwa urembo na uzuri wa Sabby ndiyo unawapa kiwewe baadhi ya wanaume wanapomuona na kumtaka kimapenzi wengine hutishia hata kutaka kumharibia mambo yake kisa kuwanyima penzi. Sabby anasema kama hawataacha tabia hiyo ya kumnyanyasa itafikia wakati atawataja majina na kuanika mesage zao za hovyo kwasababu watu hao inaonekana hawapo serious na kazi ila wapo kwenye industry kwa kutimiza tamaa zao za kimwili.

Habari zinasema kuwa kwa wakati huu Sabby anaangalia namna ya kujiimarisha kwenye film na music industry na sio kushobokea ngono !

Like our Facebook page Swahili World Planet for more updates about Tanzanian movie stars' latest gossips, news, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment