Wednesday, May 21, 2014

Ugomvi Wa Wema Sepetu Na Kajala Wafika Bungeni.

Wema na Kajala
Ule mgogoro wa mastaa wawili ambao wote ni waigizaji wa filamu nchini Wema Sepetu na Kajala Masanja umefika kwa waheshimiwa wabunge ambao wamewataka mastaa hao wawili kukaa chini na kumaliza tofauti zao na kuwa mashostito wa kutupwa kama awali. Kwa mujibu wa chanzo kimoja makini kikizungumza na Globapublishers  wabunge hao ambao wengi wanapenda sanaa wamemwambia kiongozi wa kundi la Bongo Movie Unity Steve Nyerere afanye juu chini Wema na Kajala wamalize ugomvi wao na kama akishindwa basi awaambie ili wao wawakalishe chini kwa kuwa wasanii hao wana majina makubwa na kuna chipukizi wengi wanawangalia ili kufikia walipo hivyo haileti picha nzuri kwa kuwa huko mwanzo walikuwa marafiki wazuri na mfano wa kuigwa.
"Walimwambia Steve kwamba ni kitendo cha aibu kwa mastaa wakubwa kama hao kugombana, hiyo inawapunguzia heshima kwani hiki kilikuwa ni kipindi cha kushikamana kwa umoja ili kuisogeza mbele tasnia yao badala ya kulumbana" kilisema chanzo hicho.

Nae Steve Nyerere alipotafutwa na GPL alikiri waheshimiwa wabunge kumwambia suala hilo.


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Filamu ya SIO SAWA tayari ipo madukani nunua nakala yako halisi sasa.

No comments:

Post a Comment