Wednesday, May 21, 2014

Irene Uwoya, Majid Michael, Mariam Ismail, Jose Chameleon Na Professor J Kuigiza Filamu Mpya Pamoja !

Irene Uwoya
Habari mpya ni kuwa kuna uwezekano mkubwa mastaa wa muziki na filamu Afrika mashariki na Afrika magharibi kukutana katika filamu mpya ya kitanzania ambayo story yake itahusu mambo ya muziki. Swahiliworldplanet imepenyezewa habari hii na chanzo cha uhakika ambacho ni msanii maarufu nchini  na anayetarajiwa kuwa mmoja wa waigizaji wakuu wa filamu hiyo. Kwasasa tayari zimeshafanyika seminar zaidi ya nne kufanya utafiti wa kutosha kuhusu filamu hiyo ambayo kwa mujibu chanzo hicho wanataka iwe filamu ya mwaka. Kwa mujibu wa chanzo hicho makini mpaka sasa baadhi ya mastaa waliofikiriwa kucheza filamu hiyo ni pamoja na Professor J, Irene Uwoya, Mariam Ismail(Tanzania), Jose Chameleon(Uganda) na muigizaji maarufu wa Ghana Majid Michael. waigizaji wengine watatokea nchi kama kenya na nyingine za kiafrika ambapo filamu hiyo pia inatarajiwa kushutiwa nchi mbalimbali.

Mariam Ismail na Professor J
"Wasanii wapo na mojawapo, ila bado pia majadiliano juu ya hao wasanii yanaendelea, hapa Tanzania wasanii ambao wanafikiriwa kucheza ni kama Irene Uwoya, Mariam Ismail, Professor J, Kutoka Uganda anafikiriwa zaidi Jose Chameleon, Pia muigizaji maarufu wa Ghana Majid Michael anafikiriwa sana kucheza. Na kila nchi anapotoka msanii wameona baadhi ya vipande vishutiwe huko huko ikimaanisha itakuwa ni Ugandan, Kenya, Ghana na Tanzania, finally vipande vingine vitashutiwa nchini Turkey(Uturuki) ambapo kwasasa Irene Uwoya hayupo amekwenda kwenye kazi(Uturuki) na pia kuangalia mazingira na kukubaliana na wenye mazingira hayo itakapomalizikia filamu hiyo(nchini Uturuki), huku wengine tukiendelea na Seminar juu ya filamu hiyo" Kilisema chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa jina lake.
Majid Michael
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Filamu ya SIO SAWA ipo madukani nunua nakala yako halisi sasa.

No comments:

Post a Comment