Sunday, February 23, 2014

FILAMU YA "GUMZO" KUTOKA KWA NISHA YAWA GUMZO KWELI, NCHI MBALIMBALI ZAISUBIRI KWA HAMU.

Nisha akiwa kwenye interview ya Tv
Filamu ya "Gumzo" kutoka Nisha's Film Production inatarajiwa kutoka tarehe 27 mwezi huu wa February. Kama zilivyo filamu nyingi kutoka kwa Salma Jabu Nisha tayari filamu ya GUMZO imeshakuwa gumzo kweli kwenye social media na TVs huku ikiwa bado kutoka kutokana na watengenezaji kuifanyia promo ya kutosha kama ilivyo Hollywood na Bollywood kufanyia filamu promo ya kutosha kabla haijatoka ili watu wajue kuwa kuna kazi mpya inakuja. Kwa mujibu wa Nisha ni kuwa katika Gumzo wamekuja tofauti na kazi zilizotangulia. Filamu hiyo ukiachilia mbali Nisha mastaa wengine waliocheza ni King Majuto, Wastara Juma, Hemedy Suleiman na Tausi ambaye amecheza kama mke wa Hemedy.

Vituo mbalimbali vya Tv kwasasa vinamhoji Nisha kuhusiana na filamu hiyo vikwemo TBC na Channel Ten. Interview ya Nisha na Channel Ten kupitia kipindi cha Action and Cut itaonyeshwa kesho Jumatatu saa tatu usiku. Zinazoonekana ni baadhi ya picha wakati Nisha akifanyiwa interview. Vile vile habari nyingine ni kuwa nchi mbalimbali tayari zinaisumbia kwa hamu filamu hiyo kutoka kwa Nisha.

Nisha na Tausi aliyecheza kama mke wa Hemedy katika filamu ya Gumzo.
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment