Wednesday, November 26, 2014

Nilimwaga Sugu Tukiwa Kwenye Process Za Kufunga Ndoa: Faiza Ally

Baada ya baadhi ya watu kudai Faiza Ally aliachwa na Mh. Sugu Mbilinyi sababu ya mavazi yake muigizaji huyo na mrembo wa mbio za mashindano ya Miss Tanzania miaka iliyopita kupitia mitandao yake ya kijamii Facebook na Instagram ameandika hayo hapo chini kuwa yeye ndio alimwaga Sugu na sio kinyume chake...


"Sasa leo ngoja nifunguke.... Yaani nikiweka picha zangu kwa raha zangu mnaanza kusema oh ndio maana SUGU kakimbia ndio maana kaniacha Nasema hivi MIMI NDIO NIMEMUACHA mkome kunisema nimeachana na nimemuacha tukiwa kwenye process za ndoa na tulisha kutana na padri na kwenye jumuiya nilisha anza ..... Kuna vitu vikinifanya niondoke kabla ya ndoa ambavyo vitabaki kuwa vya kifamilia ....... Nyie mna muona sugu Kama si mtu wa kawaida mm namuona Kama alie kuwa mpenzi wangu na Sasa ni baba wa mtoto wangu .... Lkn anajua ubora wangu na faida zangu Pumbavu zenu yote mnaodhani niliachwa tena kwa mavazi anajua na anapenda mavazi yangu ..... Nachukia kuamka asubuhi na kukuta comments za kusemwa vibaya.... Nyie mnajua tabia zake ????? Au mnamuona kwa mbali ?????"

No comments:

Post a Comment