Monday, November 24, 2014

Diamond Platnumz Awagaragaza P-Square Wa Nigeria



Star wa Bongofleva Tanzania Diamond Platnumz amewabwaga wasanii wa Nigeria P-Square kwa idadi ya mashabiki waliotazama video zao.
Video ya P-Square itwayo Shekini ambayo ilitoka tarehe 17 mwezi huu mpaka sasa imetazamwa na watu zaidi ya 333,000 na bado inaendelea kuhesabu wakati video mpya ya Diamond iitwayo Nitampata Wapi iliyowekwa You Tube tarehe 20 mwezi November imetazamwa na watu zaidi ya 433,000 na bado inaendelea kuhesabu. Wengi hawakutarajia kwasababu P-Square ni maarufu zaidi Afrika na video yao imetangulia siku tatu kabala ya Diamond. Hii inaonyesha Diamond kazi zake zinazidi kukua na kupata mashabiki wapya kila siku.

No comments:

Post a Comment