Monday, November 24, 2014

Cloud Agonga Mwamba Kumuangukia Frank Mwikongi.

Frank
Wiki kadhaa nyuma ziliibuka habari kuwa Cloud Issa Musa alimfanyia fitina Frank Mohamed Mwikongi katika deal la kucheza filamu Uingereza kupitia kampuni ya Didas Entertainment na mmiliki wa filamu hiyo kueleza kuwa ni kweli Cloud alimjaza maneno kibao asifanye kazi na Frank kwa amdai hajui kitu ikiwemo uongozaji wa filamu.

Sasa habari zinadai kuwa Cloud alimfuata Frank kumuomba msamaha wayamalize lakini Frank bado hajakubaliana na hilo hivyo kuendelea kukaushiana ikidaiwa si mara ya kwanza Cloud kumfanyia fitina na uzandiki Frank.

Hata hivyo wawili hao wote hawakuweza kupatikana ili kuelezea hilo.

                                                                            Cloud

No comments:

Post a Comment