Saturday, August 16, 2014

Mtitu Ajiuzulu Uongozi Club Ya Bongo Movie Unity Baada Ya Kashfa Kuikumba Club Hiyo.

Mtitu
Kufuatia kashfa mbalimbali zinazoiandama Club ya Bongo Movies Unity ikiwemo kudaiwa kuandaa dua ya kuwaombea wasanii mbalimbali waliofariki kwa maslahi binafasi leo hii mmoja wa viongozi wa Club hiyo William Mtitu ameamua kujiuzulu kufuatia kashfa hiyo ili kueouka kulitoa doa jina lake ambalo halijawahi kuchafuka kwa miaka zaidi ya kumi sasa tangu aingie katika sanaa.
Kupitia facebook Mtitu ameandika....
"Kwa kulinda heshima yangu binafsi nayakampuni yangu nimeona mimi kama MTITU nijivue rasmi leo nafasi ya uongozi na nitabaki kuwa kama mwanachama wa kawaida wa CLUB ya bongo movie sababu kiukweli SIPENDEZWI kwa asilimia kubwa na jinsi club inavyoendeshwa na sioni kama tunaelekea popote badala yake club imekuwa ni sehemu ya baadhi yetu kujipatia mkate wa kila siku kwa kutumia JINA LA
CLUB ...kitu ambacho SIKUBALIANi NACHO.
Na ikumbukwe sina ugomvi wala chuki na mtu yeyote ndani ya bongo movie....
Wacha maisha yaendelea kama zamani..
Nawatakia wèek end njema... @all"

 Mwenyekiti wa sasa wa Club hiyo ya Bongo Movies Steve Nyerere ndiye anadaiwa kuandaa dua hiyo kwa maslahi binafsi, Steve ambaye pia ameingia rasmi kwenye siasa na kutangaza kugombea ubunge mwakani jimbo la Kinondoni inadaiwa hata ushindi wake kama mwenyekiti wa kundi hilo ulikuwa wa mizengwe.

No comments:

Post a Comment