Thursday, May 8, 2014

Wema Sepetu Anasa SMS Za Mazungumzo Ya Kajala Na Clement Yule Kigogo Wa Ikulu.

Wema Sepetu
Unaweza ukaficha siri na ukaamini hakuna atakayejua bila kukumbuka kuwa hakuna siri ya watu wawili ! Hatimaye Wema Sepetu amenasa ushahidi wa aliyekuwa rafikiye kipenzi, Kajala Masanja wa kumwibia aliyekuwa bwana’ke, Clement au CK, yule kigogo wa ikulu
MIL. 13 KISINGIZIO TU
Habari za mjini kwa wiki nzima ni kusambaa kwa ujumbe mfupi (SMS) za kimapenzi za Kajala na CK ambazo sasa zimefunua kisa kamili cha mastaa hao kuhitilafiana huku Sh. Milioni 13 zikiwa kisingizio tu.
WEMA ALIKUWA ANATAFUTA USHAHIDI?
Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na mastaa hao, kupatikana kwa meseji hizo ni kama mpango wa Mungu, kwani sasa kitendawili kimeteguka.
Baadhi ya meseji zilizonaswa.
“Wema alikuwa anatafuta ushahidi kama kweli Kajala anatembea na CK hivyo sasa amepata ushahidi.
“Mwenye macho haambiwi tazama na kama hujui kusoma hata picha huoni? Ama kweli kikulacho ki nguoni mwako!” Kilisema chanzo hicho.
Habari za ndani zilieleza kuwa meseji hizo zilikutwa kwenye simu ya CK na mwanamke mwingine ambaye naye anadaiwa kutoka na kigogo huyo, aliyetajwa kwa jina moja la Naima aliyekwenda kumbwagia ‘zigo’ Wema kwa ajili ya ushahidi.
Kajala Masanja.
Ilisemekana kwamba Naima alimuomba simu CK kwa kuwa ya kwake ilikuwa mbovu.
Habari zilizidi kudai kuwa baada ya CK kumpa mpenzi wake huyo simu yake, kumbe zile meseji alizokuwa akichati na Kajala alikuwa amesahau kuzifuta ndipo zilipobambwa.
Mpashaji aliweka wazi kwamba meseji zile zilimshangaza Naima kwa kuwa yeye alikuwa ni mmoja wa watu ambao walikuwa hawaamini kabisa kama kulikuwa na ukweli wowote kuhusu tuhuma za Kajala kutembea na CK.
NAIMA ACHANGANYIKIWA
“Yaani Naima alipoziona meseji alichanganyikiwa kabisa, alikuwa kama kachomwa sindano ya ganzi kwani alikuwa ni mmoja wa watu ambao  hawaamini kabisa kama kweli Kajala anatembea na CK.
“Naima alipokaa vizuri ndipo akaanzisha timbwili lenye ujazo mkubwa na CK,” kilisema chanzo hicho.
Mnyetishaji aliendelea kutiririka kuwa katika SMS hizo ambazo zilionesha waziwazi namba ya Kajala, zilikuwa zikielezea namna CK alivyokuwa akimuomba msamaha Kajala kwa kutopokea simu yake.
HUU HAPA MZIGO
Mtiririko na meseji hizo ulikuwa hivi;
CK: “Mama mimi sipendi kukatiwa simu  pze, ok sawa lakini mi nakupenda.
Kajala: Kwa hiyo ndiyo unaniambiaje?
CK: Umeamua kuniblock?
CK: Kwa nini hupokei simu zangu?
CK: Unaponikatia simu wakati mimi naongea sijapenda sijui nijielezeje mama haya sawa.
Kajala: Fanya mambo.
Wema na Kajala
MZIGO MIKONONI MWA  WEMA
Ilisemekana kwamba baada ya Naima kuona meseji hizo alizihifadhi ili akamfikishie Wema  na kumuonesha jinsi rafiki yake alivyokuwa siyo mwaminfu kwake kitu ambacho alikifanikisha.
Habari zilidai kuwa baada ya Wema kuona SMS hizo alipatwa na mshtuko mkubwa kwani alikuwa haamini kama ni jambo analoweza kulifanya rafiki yake Kajala.
Ujumbe mwingine ulionaswa.
Baada ya ishu hiyo kuwa ndiyo habari ya mjini, Globalpublishers ilimsaka Wema ili kuzungumzia kuhusu meseji hizo.
Alipopatikana, Wema alifunguka kuwa  amesikitishwa mno na kitendo cha Kajala.
Wema alisema bora angefanya mtu mwingine yeyote lakini siyo Kajala aliyejitolea kuyaokoa maisha yake.
“Ukweli kabisa angefanya mtu mwingine yeyote wala isingekuwa ishu lakini siyo K. Aisee K amenishangaza na kuniumiza mno.
“Nilikuwa nimeshapanga niweke naye mambo sawa maisha yaendelee kama zamani lakini kwa hili siwezi kumsamehe tena,” alisema Wema aliyeonekana kukerwa na kucharuka vibaya.
HUYU HAPA MAMA WEMA
Baada ya kumalizana na Wema
GPL ilimtafuta mama Wema, Mariam Sepetu ili kuzungumzia jambo hilo ambapo alisema kuwa siku zote alimwambia mwanaye kuwa achague marafiki wa kuwa nao lakini hakulitilia maanani.
“Unajua nilikuwa namwambia Wema kila siku, achague marafiki ambao atakuwa nao. Wengine siyo marafiki wa kweli, ndiyo kama hivyo ilivyotokea, nawaachia wenyewe mimi sina la kusema,” alisema mama Wema.
KAJALA VIPI?
Hata hivyo, gazeti lilimtafuta Kajala kwa njia mbalimbali lakini lilitonywa kuwa yupo China kwa ‘biashara zake’.
Katika mahojiano maalum na gazeti pacha la hili, Ijumaa Wikienda hivi karibuni, Kajala alikana kuwa hata na namba ya CK.
“Katika maisha yangu CK niliwahi kuonana naye mara moja tu, sina hata namba yake ya simu,” alinukuliwa Kajala.
TEAM WEMA YASHANGILIA USHINDI
Kwa upande wake lile kundi linalojiita Team Wema katika mitandao ya kijamii ilijipongeza kwa kupata ushahidi huo ambao sasa umeleta sura mpya ya ugomvi wa wawili hao.
Sehemu ya maoni mengi mitandaoni ilisomeka: “Sasa kule kulia kote runingani na mwanaye matokeo yake ndiyo haya? Kama kweli Kajala kamfanyia Wema hivyo, basi anapaswa kuomba msamaha hata kama Wema yupo na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’. 

source: Globalpublisher

No comments:

Post a Comment