Monday, May 5, 2014

Sabby Angel Ajutia Uzuri Na Urembo Aliojaaliwa Kutokana Na Wanaume Wengi Kumtaka Kimapenzi.

Sabby Angel
Muigizaji mrembo wa filamu anayekuja juu kwa kasi nchini Sabby Angel ameonekana kuchoshwa na tabia za baadhi ya wanaume hasa waliopo kwenye sanaa kumtongoza kila siki tena kwa nguvu. Sabby amesema kuwa wengi ni wasanii na waume za watu mapaka inakuwa kero kwani wengine humtishia kumharibia jina kama msanii na pia kama mwanamke anapowakatalia penzi wanalotaka. Kwa mujibu wa Sabby mwenyewe sababu kubwa inayofanya wanaume wengi wamfuate mara kwa mara ni urembo na uzuri alionao kiasi cha kuwa kero hata maeneo ya ofisini.

"kwa sababu hilo ni tatizo la kweli linalonyima raha kabisaa... usumbufu ni mwingi sanaa kupita kiasi... hata baadhi ya wale wa karibu ninawaheshimu na kufanya nao kazi.. wanaomba mapenzi,
tena wengine wanasubutu kutishia kutoka fanya kazi yangu vizuri.. au kutoifanya kabisa kama nitaka kuhusika kimapenzi na wao, nimelinyamazia hili swala kwa mda mrefu sasa limenichoshaa... am tired of the unproffesionalism going on in the entertainment sector and in my all careers, wengine kutishia kuniharibia jina ili waniharibie heshma yangu kama mwanamke kisa kuwanyima mapenzi,
this problem I have faced in the film industry.... mostly... na pia kazini kiasi" Alisema Sabby Angel ambaye anatajwa kama mmoja wa wasanii wa kike wenye mvuto Afrika mashariki

Sabby ambaye pia ni mwanamuziki huku akionekana amekasirishwa na jambo hilo aliendelea kwa kusema "
YES. na naelewa kutongozwa ni lazima.. ila kinachoniuzi ni wale ninaofanya nao kazi karibu na kuwaheshimu... kunipa vitisho... kisa ngono. loh! aibu, tena watabaki midomo wazi. kwani sanaa yangu inazidi kunawiri.. na kama ni uhusiano.niliyenae ananitosheleze. siezi saliti uaminifu wa mpenzi wangu"
Sabby Angel

No comments:

Post a Comment