Wednesday, March 5, 2014

Filamu Mpya Ya Mohamed Mwikongi "Frank" Yazuiliwa na Bodi Ya Filamu.

Mohamed Mwikongi "Frank"
Star wa filamu nchini Mohamed Mwikongi maarufu kama Frank ambaye ni mmoja wa waigizaji wakongwe aliyenza kujipatia umaarufu mwanzoni mwa miaka ya 2000 anatarajiwa kuonekana na filamu mpya ya Mv Spice Islander akiwa na wasanii wenzake wenye ndani ya filamu hiyo. Hata hivyo habari za uhakika ni kuwa filamu hiyo imezuiliwa na bodi ya filamu Tanzania kwa madai baadhi ya picha za filamu hiyo zinatoka katika tukio halisi la ajali ya meli iliyowahi kutokea Zanzibar Mv Spice Islander. Hivyo bodi kuwataka wahusika wafanyie marekebisho hayo madogo ya kutumia baadhi ya picha chache halisi za tukio hilo.



Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment