Kwa upande mwingine pia wasanii hao ambao wameonyesha moyo wa kutangaza Uafrika huko Ulaya kwa kutumia lugha ya Kiswahili ambayo inazungumzwa pia nchi za Scandinavia wameingia mkataba na kampuni ya Nordisk Films ambayo ni kampuni kubwa ya usambazaji filamu katika nchi za Scandinavia hivyo wataanza kufanya kazi na kampuni hiyo. Vile vile wasanii hao pia ambao wameshafanya kazi na wasanii wa Swahiliwood(Tanzania) kama vile Lucy Komba wameingia mkataba kuhusu maeneo ya location ya filamu watakazokuwa wanatengeneza na Bolig Aalborg ambalo ni shirika la nyumba la Nordjylland na picha hapo chini zinaonyesha wakati wasanii hao walipokutana na shirika hilo kuangalia nyumba zao mpya ambazo tayari wameshajenga na nyingine bado zinajengwa kwa ajili ya kutumia kama location wakati wa kutengeneza filamu.
VAD likiwa na maana ya Voice Of Africa In Denmark ilianzishwa mwaka 2011 na inapokewa msanii yeyote mwenye nia ya dhati katika kuitangaza Afrika kupitia sanaa ya filamu na mwenye kipaji cha uigizaji bila ubaguzi wowote.




No comments:
Post a Comment