Monday, August 26, 2013

SLIM OMAR KUVUTA JIKO MUDA SI MREFU.

Slim Omar ambaye ni muigizaji anayefanya vizuri kwasasa katika filamu amesema kuwa ana mpango wa kuoa hivi karibuni. Slim anayetamba na filamu nyingi sokoni amesema kuwa umri alionao ni muafaka kwa kuvuta jiko na mchumba tayari anae ambaye pia wanaelewana vizuri tu na hampi shida katika masuala ya kazi zake za filamu. Akizungumza na Swahiliworldplanet Slim alisema "mungu akipenda soon siunajua wakati muafaka na umri wangu inapendeza niwe na mke wa ndoa mapema iwezekanavyo". Aliongeza kwa kusema kuwa "mchumba tayari ninae tena kitambo wala sina kelele na watu na wala hajulikani pia ni tofauti na mambo yetu, namuelewa ananielewa vizuri nafanya kazi safi"

We wish him all the best........

Like our facebook pages Swahili World Planet Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news

No comments:

Post a Comment