Friday, August 30, 2013

MTASUBIRI SANA SIMUACHI DIAMOND HATA KWA DAWA: PENNY.

Peniel Mungilwa(Penny) mtangazaji wa DTV ambaye pia ni mpenzi wa mwanamuziki matawi ya juu Diamond Platinumz amesema kuwa licha ya maneno mengi yanayosemwa lakini hawezi kumuacha Diamond. Hivi karibuni ziliibuka habari kuwa Diamond ana demu mwingine wa Kenya anayeitwa Angel Maggie ambaye ameapa kumpa Diamond penzi zito la kukata na shoka hivyo watu kujua Penny na Diamond kinaweza kunuka muda wowote. Akizungumza na GPL Penny alisema “Yatasemwa mengi lakini siwezi kumuacha Diamond, namuamini na najua haya yote yanayotokea ni kwa sababu ya kazi yake kwa hiyo wanaodhani mimi nitayachukua na kuamua kumuacha watasubiri sana, ndiyo kwanza penzi letu linazidi kushamiri,” alisema Penny. 

                       Penny na Diamond

 Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment