Saturday, August 24, 2013

MODEL MWAJABU JUMA KUJITOSA KATIKA MUZIKI WA BONGOFLEVA.

Mwajabu Juma ambaye ni model na video vizen amemua kujitosa katika muziki wa Bongofleva kwa kuwa kipaji cha kuimba anacho muda mrefu ila alikuwa akisubiri muda ufike. Akizungumza na Swahiliworldplanet mrembo huyo ambaye anaonekana katika video ya Yahaya ya Lady Jaydee amesema kuwa sababu nyingine ni kuwa modelling pia bado haijampa mafanikio anayoyataka hivyo ameamua kujitosa katika music wa RnB na kwasasa yupo katika mazoezi kabla ya kuachia ngoma yake ya kwanza.

Mwajabu aliyejaaliwa mvuto alishinda taji la Miss Tanzania top model 2011 na kuingia kwake kwenye music kutaongeza idadi ya wanamuziki wa kike ambao bado ni wachache ukilinganisha na wanaume.


                                  Mwajabu akiwa katika pose la swimsuit........
Like our facebook pages Swahili World Planet Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news

No comments:

Post a Comment