Thursday, August 15, 2013

LULU KUZINDUA RASMI FILAMU YAKE YA FOOLISH AGE MLIMANI CITY, LADY JAYDEE KUMSINDIKIZA.

Inaonekana actress maarufu nchini Elizabeth Michael(Lulu) amepania kufika mbali katika tasnia ya filamu. Muigizaji huyo ameweka wazi kuwa atafanya uzinduzi wa filamu yake ya "Foolish Age" tarehe 3o mwezi huu wa nane katika ukumbi wa Mlimani City na wasanii mbalimbali wakiwemo wanamuziki kama Lady Jaydee na Machozi Band kutarajiwa kushusha burudani ya kufa mtu. kupitia mtandao mmoja wa kijamii Lulu aliyejaaliwa kipaji cha kuigiza na mvuto aliandika "Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu....!!!ninafuraha ya kuwafahamisha kuwa TAREHE 30/8/2013 ndio siku nitakayozindua movie ya mpya ya FOOLISH AGE....hatimaye narudi kazini!!!!Uzinduzi utafanyika katika ukumbi wa MLIMANI CITY....kutakuwepo na wasanii mbalimbali wa muziki....na pia LADY JAY DEE pamoja na MACHOZI BAND atakuwepo pia!!!nahitaji support ya mashabiki wote wa LULU na mashabiki wa BONGO MOVIE.....♥♥♥♥!!!#PROINPROMOTERS"

  Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies swp for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news

No comments:

Post a Comment