Wednesday, April 17, 2013

NDOA YA IRENE UWOYA YAVUNJIKA, ATENGWA NA FAMILIA YAKE, NDIKU AZIMIA KISA ISSUE YA UWOYA NA DIAMOND.

News is that ndoa ya actress Irene Uwoya na mumewe Hamad Ndikumana imevunjika rasmi Uwoya mwenyewe akiwa amemwambia hivyo mwandishi wa globalpublishers. Uwoya alisema kuwa mumewe alizimia baada ya kusoma habari ya yeye na Diamond kufumwa hotelini pamoja siku chache tu baada ya kudaiwa kurudiana na mumewe, Ndiku alipozinduka alirudi kwao Rwanda huku akitamka kuvunjika rasmi kwa ndoa yao hiyo. kwa upande mwingine Irene amesema ametengwa na familia yake kutokana na issue hiyo na hawataki kumsikia Diamond kabisa na Uwoya pia hataki kumsikia mwanamuziki huyo ambaye ndio chanzo cha yote. Tangu wafunge ndoa ya kifahari na mumewe mwaka 2009 ndoa yao inadaiwa kuwa na migogoro ya mara kwa mara huku Uwoya akidaiwa kutotulia katika ndoa yake ilihali mumewe anadaiwa kumpenda sana. ili kusoma mahojiano ya actress huyo na globalpublishers ingia hapa www.globalpublishers.info

                                                    Back to their wedding in 2009

No comments:

Post a Comment