Thursday, June 19, 2014

William Mtitu Amuandikia Ujumbe Mzito Florah Mbasha Kuhusu Tuhuma Za Mumewe Kubaka.

Muigizaji, producer na director wa filamu nchini William Mtitu amemfungukia Florah Mbasha ujumbe mzito kuhusiana na sakata la ubakaji linalomhusu mumewe kwasasa. Kupitia mtandao mmoja wa kijamii Mtitu ameandika

“Ukiiangalia vizuli hii picha utagundua kitu katika macho ya Florah Mbasha kuna kitu nakiona kimejificha lakini sasa hivi kimeshajitokeza tayari.....hicho kitu ndicho kilichompeleka jela Mbasha na asipokuwa makini anaweza asiwe uraiani tena kama ilivyowatokea familia ya Nguza .namaanisha mzee Nguza na Papii Kocha wako wapi? Kiukweli Florah una roho mbaya ya mwisho kabisa ilichanganyika na ukatili wa mwisho kabisa kiasi kwamba nashindwa kuelewa umeokoka nini wewe ? Eti umemrudia YESU ?YESU yupi huyu ninayemwabudu mimi au una YESU wako wewe na HUYO GWAJIMA wako? Leo umemsahau Mbasha wewe ? Wakati alikuokota umechakaa wakati Mbasha dereva teksi leo wataka kumfunga ili iwe nini sasa Mbasha akifungwa utapata faida gani wewe? Huyo mtoto akija kukuuliza baba yuko wapi utamwambiaje? Fine unaweza kujikaza ukamwambia yuko jela je akikuuliza nani alimshitaki utajibu nini ?

 Pia waweza kujikaza ukawataja hao wasichana mliowapandikiza je akiuliza wewe ulifanya jitihada gani baba asifungwe utasemaje? Hapo hauna jibu acha roho mbaya NENDA KAMTOE MARA MOJA NA MWENDE NYUMBANI MKAONGEE KAMA FAMILIA TWAJUA UWEZO HUO UNAO ILI NA YEYE ATAFUTE HAMSINI ZAKE KAMA WEWE ULIVYOAMUA KUJISALIMISHA KWA GWAJIMA. USIJE UKASHANGAA WATU WAKASUSIA KAZI ZAKO ZOTE. GDAY"

Florah na mumewe Emmanuel Mbasha kabla ya kuingia katika gogoro zito
Like our Facebook page Swahili World Planet for more updates about Tanzanian movie stars' latest gossips, news, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news

No comments:

Post a Comment