Saturday, June 21, 2014

Wema Sepetu Afunguka Kwa Uchungu baada Ya Kutukaniwa Mama Yake Mzazi.

Wema
Wema Sepetu ameonekana kufungukia wale wanaomtukana kila siku na sasa kufikia hatua ya kumtukania hadi mama yake mzazi, Kupita mtandao mmoja wa kijamii Wema amefunguka kwa uchungu kwa kuandika
 "Dah...! Sijui hata niseme nini...! Ila si mlitaka kuniumiza... leo mmefanikiwa... nawapeni hongera.... Tena mmetisha haswa... Kila sjku huwa hata siumizwi na matusi yenu cuz naonaga kama ni mnajisumbua tu... Hakuna siku nimelia kwa uchungu kama leo... I min mnitukane mimi mpaka mchoke but leave my mum out of it... Kawakosea nini nyinyi mama angu mpaka mfanye hivyo... Mzazi nwenyewe ndo nimebakia nae mmoja tu... mnataka afe na yeye nibaki yatima sio... dah... leo mmeniweza... saana jamani... Basi naomba isifike huko... nina uchungu sana na mama angu ... nampenda sana mama angu ila naona mnataka kuniulia mama angu... Picha halisi ndo hio hapo juu kweli mtu uende ukamfanyie hivyo mama wa mwenzako... una mama wewe.. au uliokotwa na hujui uchungu wa mama... dah... nime surrender leo.... hongera zenu narudia tena... mmeniweza leo.... dah... Mungu nipe nguvu ktk hili jamani... Kwani nilichokikosea haswa ni kitu gani mpaka iwe hivi . Nimekosa nini mimi yarabi toba.... Eeeh mungu... Dah... Ila nashkuru..."

Sisi tunafikiri sio tabia za kistaarabu katika ugomvi binafsi kuwaingiza wazazi na kuwatukana, ni ukosefu wa maadili na kutokustaraabika. pole sana Wema Mungu atawahumu waliokutukania mzazi wako.
mama Wema


Like our Facebook page Swahili World Planet for more updates about Tanzanian movie stars' latest gossips, news, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news


No comments:

Post a Comment