Tuesday, June 17, 2014

Ray Na Chuchu Hans Wafunga Ndoa Kimya Kimya ! Johari Amrushia Chuchu Vijembe.

Ray na Chuchu Hans
One of the most talked about celebrity couple in Tanzania Ray na Chuchu Hans wanadaiwa kufunga ndoa kimya kimya na kuanza kuishi pamoja. Chanzo kimoja ambacho ni msanii wa filamu kimeipenyezea Swahiliworldplanet habari hiyo leo hii wakati alipoenda kwenye interview ya Radio moja na kuambiwa na mtangazaji wa kipindi kinachohusu wasanii ingawa habari hiyo bado kusambaa hivyo Swahiliworldplanet imeamua kukupakulia gossip hii ikiwa bado ya moto !. Vile inadaiwa kuwa hivi majuzi Johari anayedaiwa pia kuwa aliporwa Ray na Chuchu Hans alikuwa anamrushia Chuchu vijembe vyenye uzito wa maana katika msiba wa George Tyson huku Ray akidaiwa kumkingia kifua Chuchu baada ya kukoshwa na penzi la Chchu ambaye alikuwa Miss Tanga na Miss Tanzania talent 2005.

"kwa tetesi za chini ya carpet zinadai Chuchu Hans wameona na Ray kimya kimya na wanaishi pamoja, nimedokezwa sasa hivi na ....(akimtaja msanii mmoja ambaye kwasasa filamu yake mpya imekuwa habari ya mjini) nilikuwa nae, inasemekana Johari alikuwa akimpiga vijembe Chuchu Hans kwenye msiba wa George Tyson na Ray kumsimamia Chuchu"

Swahiliworldplanet imejaribu kumtafuta Chuchu ili kutolea ufafanuzi madai hayo lakini haikufua dafu, lakini mara nyingi Chchu na Ray wamekuwa wagumu kuanika mambo yanayohusu uhusiano wao kwenye media., Ray wiki kadhaa nyuma alisema siwezi kumuoa Chchu na siku kadhaa baadaye Chuchu akajitokeza kujibu mapigo kuwa ni lazima Ray anioe.
                                                          Ray na Chuchu Hans
Like our Facebook page Swahili World Planet for more updates about Tanzanian movie stars' latest gossips, news, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news

No comments:

Post a Comment