Sunday, March 9, 2014

Cheche Achemka Kwenye Red Carpet Ya Africa Magic Viewers Choice Awards 2014.

Star wa Siri Ya Mtungi Juma Rajabu maarufu kama Cheche jana alikuwa Lagos, Nigeria ambako tuzo za Africa Magic Viewers Choice Awards 2014 zilifanyika. Cheche alikuwa na team ya Siri Ya Mtungi ambayo ilipendekezwa kuwania tuzo kadhaa kupitia series hiyo akiwemo Cheche mwenyewe ambaye alipendekezwa katika kipengele cha muigizaji bora wa kiume wa mwaka. Tanzania haikubahatika kushinda hata kipengele kimoja huku Kenya ikitwaa tuzo tano.


Hata hivyo kwenye red carpet Cheche alichemka katika uvaaji, star huyo alivaa tshirt nyeupe, kizibao na pensi ya asili ya kitenge na chini akamalizia na raba nyeupe. Kwa ujumla cheche alipendeza lakini mavazi yake hayakuendana na event husika. Afadhali hata ingekuwa ni red carpet ya muziki au tuzo za muziki kuliko AMVCAs. In short Cheche alitokota !.....jionee hapo chini



Cheche akiwa na team ya Siri Ya Mtungi akiwemo director John Riber na Rehema Samo

Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment