Friday, November 29, 2013

FILAMU YA AFTER DEATH KWA AJILI YA KUMUENZI KANUMBA ILINIINGIZIA HASARA KUBWA: JACKLINE WOLPER


Wolper
Jackline Wolper ambaye ni star wa filamu nchini amefunguka kuwa filamu yake aliyoitoa kumuenzi marehemu Steven Kanumba iitwayo After Death ilimlostisha kwa kuwa ilimpatia hasara kubwa. Akizungumza na Globalpublishers Wolper ambaye anafanya vizuri kwasasa katika filamu alisema
"Nilitengeneza ile filamu kwa hela nyingi kidogo, kama milioni 35 au 40, nikafanya na uzinduzi pale Leaders Club uliogharimu kama milioni 13 hivi, lakini nilipokwenda kwa Wahindi wakanipa shilingi milioni 25, yaani inakatisha sana tamaa"

Alisema hasara aliyoipata na ambayo hata wasanii wenzake huipata inatokana na uwepo wa wasambazaji wachache wa kazi za wasanii, kitu kinachowafanya watu hao kujipangia bei bila kujali gharama ambazo wasanii wameingia katika utengenezaji wake.

                                                        Cover la filamu hiyo

Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment