Wednesday, October 16, 2013

NINATONGOZWA SANA NA WANAUME WENYE PESA ZAO NA NAFURAHI SANA: LULU

Actress mwenye jina kubwa Swahiliwood Elizabeth Michael(Lulu) amesema kuwa tangu atoke gerezani amekuwa akitongozwa sana na wanaume hasa wale wenye pesa zao lakini yeye huishia kufarijika kwa kupendwa. Akizungumza na mpekuzi Lulu alisema "Ninatongozwa sana na wanaume tena wenye pesa zao. Binafsi nafurahi sana kupendwa na ninapogundua kuwa mtu flani ananipenda huwa najisikia faraja sana"

Star huyo wa filamu za Foolish Age, Oxgen, Ripple Of Tears na Family Disaster aliongeza kwa kusema "kutongozwa kwa mwanamke yeyote mzuri ni jambo la kawaida. Kukubali au kukataa ombi la mwanaume ni maamuzi ya mtu binafsi, niliporejea uraiani kasi ya kutongozwa imezidi sana tofauti na nilivyokuwa nadhani"

                                                                 Lulu
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news

No comments:

Post a Comment