Pages

Saturday, November 15, 2014

Jackline Wolper Afunguka Kwa Undani Issue Ya Kumsaliti Kajala Kwa Wema Sepetu.

Hivi juzi gazeti moja la Globalpublishers lilikuwa na habari inayoonekana katika kicha cha habari gazetini hapo chini kikisema kuwa Jackline Wolper kamsaliti Kajala Masanja ambaye ni rafiki yake wa karibu kwa kitendo cha Wolper kuwa karibu na Wema Sepetu katika birthday ya Aunty Ezekiel. Baada ya habari hiyo kutoka Wolper amejibu kwa kuandika haya hapa

"kuna ule usemi wenzio wakigombana shika jembe ukalime...lakini pia ukisikiliza ya jirani utakuja kujikuta wewe ndo mnafiki na huongei na kila mtu. haya sasa watu wakigombana ni vyema uyaache kama yalivyo wakipatana usipate Aibu..sidhani kama ni sawa vyombo vya habari au Instagramers kutoa mtu akigombana na mtu basi wote mumchunie.. je ni sawa? kzma ni sawa basi ibaki kuwa sawa lakini  kwangu siyo sawa so isitegemewe mtu akizinguana na mtu me nitamkalia kimya kisa hawasemezani, no no sipo hvyoo na ndo maana kipindi cha Wema na Penny nilikua naongea na kila mtu na sasa wamepatana bado ipo vile vile, sasa nyie wagombanishi aibu yenu aibu yao......hebu msiwe na visebusebu vyakufwata maisha ya watu baki kuwa shabki tu kama unapenda wote penda wote hata kama wamegombana..kama unapenda mmoja baki hukohuko..Chama cha Amani kidumu🙌🙌 Malezi ya wazazi ndo yalonifunza hayo basi kwa leo.."


No comments:

Post a Comment