Pages

Monday, April 7, 2014

Wasanii Walaani Kanumba Kuenziwa Kwa Bonanza La Muziki Kwa Kiingilio Wakati Hakuwa Mwanamuziki.

Leo ni siku ya kumuenzi aliyekuwa muigizaji maarufu wa filamu nchini hayati Steven Kanumba ikiwa ni miaka 2 tangu afariki dunia. Leo kuna bonanza la muziki la kumenzi Kanumba huku watu wakiingia kwa kiingilio kitu ambacho baadhi ya wasanii wenyewe wamesema sio sahihi hata kidogo bali watu wachache wanataka kumuenzi Kanumba kwa kujiingizia pesa. Baadhi ya wasanii waliondika kulalamikia hilo ni wasanii wa siku nyingi nchini Michael Sangu "Mike" na Swebe.

"NIJUAVYO MIMI KANUMBA ALIKUWA MWANAKWAYA WA KANISANI AKUWAI KUWA MWANAMUZIKI WA JAHAZI WALA WA TWANGA PEPETA IWEJE TUMUENZI KWA HAYO? JAMANI PESA ZINATAFUTWA KWELI ILA KWA NJIA HIYO YA KANUMBA SIO VIZURI WATANZANIA WENGI WANASIKITIKA SANA JAMANI ? HII NI AIBU KUBWA SANA KWA FAMILIA NA KANISA ALILOKUWA AKIABUDU KANUMBA" ameandika Mike

Nae Swebe ameandika "R.I.P RAFIKI YANGU MPENDWA.. MIAKA 2 SASA.. HAUKO TENA NASI NA HAITOTOKEA... UMEKUA MTAJI KWA WALIO HAI... BADALA YA KUOMBEWA DUWA WATU WANASHEREHEKA KWA MABENDI KUYAALIKA HUKU VIINGILIO VIKITAWALA... AMA KWA HAKIKA UKISTAAJABU YA MUSA UTAYAONA YA FIRAUNI.... HUKO ULIKO SALAMU ZANGU NAZITUMA... KWA SASA FILAMU ZINAUZWA KWA MAJINA NA SURA NA SI UWEZO... YOTE KWA YOTE SOKO LA FILAMU LIMEKUFA BONGO.... ZANGU DUA ZITAKUFIKIA NA MUNGU MWENYE SIFA YA KUSAMEHE AKUSAMEHE.. NA WANAOFANYA DHIHAKA JUU YA HILI NAO AWASAMEHE.... HAKIKA.. KWA MUNGU SOTE TUTAREJEA.... NINA MENGI.. LAKINI KWA HAYA MACHACHE WACHA TUU NIJIFUTE CHOZI NA DUA KUKUOMBEA.... R.I.P RAFIKI YANGU MPENDWA STEVEN CHARLES KANUMBA"

Swebe ambaye aliigiza tamthilia na filamu kadhaa na Kanumba aliongeza kwa kuandika " R.I.P.... STEVEN CHARLEZ KANUMBA... ILA NATAMKA KWA HERUFI KUU.. NDG, JAMAA, NA MARAFIKI WAMEKUSALITI... KWA SABABU YA PESA... WACHACHE TUTAKUOMBEA UPUMZIKE KWA AMANI... KWA SABABU TUKO MAPITONI TUNAPITA... WENGI LEO WANATOA PESA ZAO KWENDA KUCHEZA MUZIKI ULIOANDALIWA KWA AJILI YA KUMBUKUMBU YAKO BADALA YA KUKUOMBEA MAPUMZIKO YA MILELE... HAKIKA WATAFANYA YAMCHUKIZAYO MUUMBA.. WATAKUNYWA, WATAPIGANA, NA HATA KUFANYA YASIYOSTAHILI ILIMRADI TUWAONE KWENYE MAGAZETI YAO NA KASHFA WALIZOZIZOEA... MUNGU ATAWALIPA KWA WAYAFANYAYO.... NAMUOMBA MUNGU AKUWEKE MAHALA PA AMANI NA KUKUPA MAPUMZIKO MEMA.. AAMEN.. ........KAMA UNAUNGANA NAMI..LIKE.. AU COMMENT ..AMEN.. PUMZIKA KWA AMANI STEVEN CHARLES KANUMBA."



Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

No comments:

Post a Comment