Pages

Friday, February 21, 2014

UZURI WA BATULI WADAIWA KUWACHANGANYA WABUNGE NA MAWAZIRI HUKO DODOMA.

Batuli
Uzuri na urembo alionao actress maarufu Swahiliwood, Yobnesh Yusuph(Batuli) unadaiwa kuwadatisha baadhi ya mawaziri na wabunge huko Dodoma. Chanzo kimoja ambacho pia ni msanii wa filamu nchini kilichodai kipo Dodoma kwasasa kwa issue zake binafsi kiliutonya mtandao huu kuwa waheshimiwa wawili wamedatishwa na uzuri wa Batuli na wanasaka mawasiliano yake ya simu lakini kwa kificho ili media hasa magazeti ya udaku yasijue na kuanza kuandika habari hizo. "Batuli yupo Dodoma kwa shughuli za Bunge la katiba na kuna baadhi ya waheshimiwa wamedatishwa na uzuri wake lakini hawajajua namna ya kumpata ili kujaribu bahati yao,Batuli ni mrembo sana siyo used kama baadhi ya mastaa wenzake so wale wabunge wamedata" kilisema chanzo hicho


Chanzo hicho kiliendelea kwa kusema kuwa kilikutana na waheshimiwa hao wawili kwa nyakati tofauti katika hoteli moja iliyopo Dodoma na kumuomba awasaidie namba ya Batuli kwa madai urembo wake unawanyima usingizi "me nipo Dom kwa issue zangu binafsi nimekutana na waheshimiwa wawili(hakuwataja majina) wame-data na uzuri wa Batuli wakataka niwape namba yake nikawaambia sina, mie sipo karibu na Batuli"

Baada ya kuzipata habari hizo Swahiliworldplanet ilimtafuta Batuli na kumueleza kuhusu habari za uzuri na urembo wake kuwachanganya baadhi ya waheshimiwa huko Dodoma, star huyo wa filamu za Bad Luck na 5 Days Family alijibu huku akionyesha kushangazwa na habari hizo kwa kusema "sikwenda Dodoma kufanya uhuni kama baadhi ya mastaa wenzangu wafanyavyo wanapokuwa Dodoma, sina uhakika kuwa namba yangu ya simu ilikuwa inatafutwa na wabunge/mawaziri kwasababu kila kiongozi tuliyekutana nae hakutoka nje ya topic kabisa vile vile sikuwa peke yangu tulikuwa wengi zaidi ya 12 na kila kikao tulikaa wote kwa pamoja"

Batuli ambaye ni mmoja wa mastaa wa filamu nchini waliojipatia umaarufu kwa kazi zao na sio skendo kama baadhi ya mastaa wenzake alimalizia kwa kusema "watu huzusha maneno kutokana na mitazamo yao ila ni vyema mtu kuongea lenye ukweli, binafsi sijaona kiongozi aliyekuwa na muda wa kupoteza kwa ufupi waheshimiwa wote wapo busy sana, sisi wenyewe tulikuwa hoi kwa vikao kuna wakati tulikuwa tunamaliza vikao saa 6 usiku, kwa ufupi naweza kusema aliyefikisha taarifa hakufanya research kutosha, vile vile tuliochaguliwa kwenda Dodoma hasa hasa kwa upande wa wasichana ni mimi na Monalisa hivyo unaweza kupata picha halisi ya tuliochaguliwa na muonekano wetu mbele ya jamii"

                                                                       Batuli
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news, life styles news and more

2 comments:

  1. Batuli mzuri sanaaa kina Wema na Uwoya watasubiri sana

    ReplyDelete
  2. Kiukweli ni kifaa cha kuuliwaza mwili na moyo.

    ReplyDelete