Pages

Thursday, December 12, 2013

WEMA SEPETU ALITAKA NIWE KUWADI: PRODUCER

Wema Sepetu

Baada  ya kudaiwa kufanya ngono katika magari ya Kampuni ya Endless Fame inayoongozwa na Wema Issac Sepetu, Prodyuza, Rashid Mohammed ‘Chid Classic’ amefunguka na kusema chanzo cha yote ni mshahara  na ukuwadi ndani ya kampuni hiyo wala siyo uzinzi.

Akizungumza na Globalpublishers Chid amesema hajafukuzwa katika kampuni hiyo kama alivyodai mratibu wa kampuni hiyo, Petit Man bali ameondoka baada ya kuchoka  kufanya kazi bila ya kulipwa mshahara.
"Ni uongo kusema kwamba nimenaswa nikifanya uzinzi Coco Beach nikiwa ndani ya magari ya Wema, sijawahi hata siku moja kufanya hivyo kwani nina kwangu ambako nina uwezo wa kumwingiza mwanamke wakati wowote,” alisema.

"Tangu kampuni ianzishwe haijawahi kulipa mishahara unadhani nitakuwa na moyo wa kufanya kazi, sikwenda pale kufanya ukuwadi kama wengine, tena nawaomba wasiendelee kusema uongo kwani nina mengi nayajua ya Endless Fame,” aliongeza Chid.
Baada ya kusikia maelezo hayo, mtandao huo  ulimtafuta Wema bila ya mafanikio ndipo likaongea na meneja wake, Martin Kadinda na alisema
"Nina wasiwasi na kauli za Chid kwanza tatizo siyo mshahara na hayo masuala ya ukuwadi ni uongo na uzushi, kama ni kweli kwa nini asiongee siku zote hadi lilipoibuka hili la kunaswa akifanya uzinzi kwenye gari?"
                                                             Chid Classic
Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

1 comment: