Tuesday, December 17, 2013

MR.NICE APATA NAFASI YA KUCHEZA FILAMU NCHINI DENMARK NA WASANII WA VAD PRODUCTIONS.

Mr. Nice kutoka Tanzania ambaye ni msanii wa muziki wa kizazi kipya aliyewahi kujipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi akiwa na style yake ya Takeu kupitia nyimbo kama Kidali Po na Kikulacho amepata nafasi ya kucheza filamu huko Denmark kupitia wasanii wa VAD productions wenye asili ya kiafrika hasa kutoka nchini Congo ambao hufanya kazi na wasanii wa nchi za Afrika hususani Afrika mashariki.

Mr. Nice amepata nafasi hiyo huku akiwa hajawahi hata siku moja kucheza filamu nchini Tanzania na dalili za kucheza filamu Swahiliwood zikiwa bado hakuna. Wasanii wa VAD kwa ujumla wamefurahi kuwa na MR. Nice nchini humo.

Angalia picha za uchukuaji wa filamu hiyo na nyingine ambazo sio za uchukuaji wa filamu hiyo.....

Follow us on twitter Swahili World Planet  and Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, beauty, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news.

No comments:

Post a Comment