Pages

Friday, August 23, 2013

SNURA AKANA TUHUMA ZA KUJIUZA KWA WANAUME WENYE PESA.

Snura Mushi ambaye ni star wa filamu Swahiliwood na katika muziki wa Bongofleva pia amesema kuwa kwa muda mrefu amekuwa akiumizwa na wanaosema kuwa njia kubwa inayompatia pesa ni kujiuza kwa mapedeshee na pia kuwauza wasichana wengine. Snura alisema kuwa kutokana na tuhuma hizo za kuzushiwa kujiuza kuna mtu pia aliwahi kutumia picha yake kwa kumnadi kwa wenye pesa lakini alishindwa kufikia malengo kwa kuwa hakumtaarifu Snura mwenyewe ambaye hana mpango huo.

Snura ambaye kwasasa anatamba na wimbo wa Majanga alisema kuwa yeye anaingiza pesa kihalali kwa kufanya kazi kwa bidii na sio kama wazushi wanavyompakazia kuwa anajiuza kwa wenye pesa.

                                                              Snura
Like our facebook pages Swahili World Planet and Bongomovies SWP for more updates about Swahili movies latest news, gossip, celebrities, features, fashions, music plus Hollywood, Bollywood and Nollywood news

No comments:

Post a Comment